Kiwanda cha silaha cha Degtyarev na Mfuko wa utafiti katika mustakabali wa Russia vimesanifu kwa pamoja roboti ya vita ya "Nerekhta-2".
Roboti hii inayofanana na kifaru kidogo ina urefu wa mita 2.5, upana wa mita 1.6 na kimo cha mita 0.9, na uzito wake ni tani 1 hivi.
Roboti hii inaweza kufanya doria, kuchunguza, kusaidia mapambano, kufanya mawasiliano, na kusafirisha watu na vitu. Ina bunduki moja nyepesi yenye kipenyo cha milimita 7.62 na bunduki moja nzito yenye kipenyo cha milimita 12.7. Watafiti pia wanapanga kuweka mzinga mdogo kwenye roboti hii.
Askari wanaweza kuwasiliana na roboti hii kwa remote kwa umbali wa kilomita 3. Pia inaweza kuendeshwa kwa maneno au ishara ya mikono. Askari akitaka roboti hii kumsaidia, anatakiwa kupunga silaha yake kwa njia maalum, baadaye roboti inafyatulia risasi kitu au mtu aliyelengwa.
Mchana roboti hii inaweza kutambua shabaha iliyoko umbali wa kilomita 5 kutoka mahali ilipo kwa darubini, na usiku inaweza kutambua shabaha iliyoko kilomita 4 kwa kifaa cha kuonea usiku.
Roboti hii ina injini yenye nguvu kubwa, na inaweza kuendeshwa kwa kasi ya kilomita 32 kwa saa. Inapofanya kazi ya usafirishaji, inaweza kubeba vitu vyenye uzito wa kilo 700.
Askari mmoja anaweza kuziongoza roboti 18 kufanya kazi kwa pamoja kwa remote moja tu.
-
Kulitokea kizaazaa mapema wiki hii jijini Nairobi baada ya jamaa mmoja kujipata kwenye njia panda. Jamaa huyu amekuwa na mpenzi wa Facebook ...
-
Kundi la wadukuzi wa mitandaoni la Anonymous limeshambulia tovuti ya wizara ya mambo ya nje ya Kenya na kuiba data muhimu, tovuti moja ya us...
-
Aliyekuwa jambazi sugu na mwizi wa majeneza jijini Nairobi John Kibera ameshindwa kuhudhuria mazishi ya mtu yoyo...
-
MUHALIFU WA BENKI MWENYE AKILI KULIKO WOTE (THE MOST PROLIFIC BANK ROBBER).. (Taarifa ya Kusisimua). Mwaka 2021 ulimwengu utashuhudia m...
-
RAHISISHA BIASHARA ZAKO, UKUE NA KUENDELEA ZAIDI KIBIASHARA KWA KUTUMIA PROGRAM MPYA YA KUENDESHEA BIASHARA YA StraightBook PROGRAM HII INAK...
-
The World Humanitarian Summit held in Istanbul, Turkey on 23 and 24 May 2016 saw 9,000 delegates from governments, United Nations agenc...
-
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu ...
-
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema idadi ya namba tambulishi ambazo zilikuwa hazina viwango zimeendelea kupungua kutoka asilimia...
-
Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump amekejeliwa mtandaoni baada ya kuonekana akiboronga akitamka Tanzania wakati wa kutoa hot...
0 comments:
Post a Comment