Kiwanda cha silaha cha Degtyarev na Mfuko wa utafiti katika mustakabali wa Russia vimesanifu kwa pamoja roboti ya vita ya "Nerekhta-2".
Roboti hii inayofanana na kifaru kidogo ina urefu wa mita 2.5, upana wa mita 1.6 na kimo cha mita 0.9, na uzito wake ni tani 1 hivi.
Roboti hii inaweza kufanya doria, kuchunguza, kusaidia mapambano, kufanya mawasiliano, na kusafirisha watu na vitu. Ina bunduki moja nyepesi yenye kipenyo cha milimita 7.62 na bunduki moja nzito yenye kipenyo cha milimita 12.7. Watafiti pia wanapanga kuweka mzinga mdogo kwenye roboti hii.
Askari wanaweza kuwasiliana na roboti hii kwa remote kwa umbali wa kilomita 3. Pia inaweza kuendeshwa kwa maneno au ishara ya mikono. Askari akitaka roboti hii kumsaidia, anatakiwa kupunga silaha yake kwa njia maalum, baadaye roboti inafyatulia risasi kitu au mtu aliyelengwa.
Mchana roboti hii inaweza kutambua shabaha iliyoko umbali wa kilomita 5 kutoka mahali ilipo kwa darubini, na usiku inaweza kutambua shabaha iliyoko kilomita 4 kwa kifaa cha kuonea usiku.
Roboti hii ina injini yenye nguvu kubwa, na inaweza kuendeshwa kwa kasi ya kilomita 32 kwa saa. Inapofanya kazi ya usafirishaji, inaweza kubeba vitu vyenye uzito wa kilo 700.
Askari mmoja anaweza kuziongoza roboti 18 kufanya kazi kwa pamoja kwa remote moja tu.
-
Corruption and economic turmoil often go hand-in-hand. In western nations like the United States and many European countries, we often see c...
-
Mr Museveni says Uganda will remain at peace. Nobody has the capacity to disturb peace. Nobody has the capacity to disturb this, however muc...
-
IDADI ya Watanzania wanaosubiri kunyongwa imekuwa ikiongezeka na hadi sasa imefikia 465 kutokana na hukumu ya kifo kutotekelezwa tangu mwaka...
-
The Zika virus strain linked to surging cases of neurological disorders and birth defects in Latin America has now been found in Africa, ...
-
This density map of the cerebral cortex of a mouse shows which neurons get activated when the animal explores of a new environment. The l...
-
So you are walking around town, minding your own business when all of a sudden there is some commotion. Looking around, you notice ...
-
At least 12 people have been confirmed dead and scores still missing following a landslide that hit Bundibugyo district Tuesday morning. Hun...
-
A son of former Imperial Bank chairman Alnashir Popat, and three other Kenyans have been named among individuals with companies registered i...
-
A lawmaker was charged on Tuesday with fraud at a Milimani court. Kitui Rural MP Charles Mutisya Nyamai, who had a pending warrant of arrest...
-
Askari: Haloo afande… Lango 115 nimemkamata akiwa amevuka ‘zebra cross’ wakati namtaka ‘assign’ kwa kosa alilofanya akaanza kunitukana… anas...
0 comments:
Post a Comment